• Malalamiko |
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za Watumishi |
MADABA DISTRICT COUNCIL
MADABA DISTRICT COUNCIL

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Madaba

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhamira
  • Utawala
    • Muundo wa Utawala
    • Department and Section
  • Investment
  • Huduma
    • Huduma ya Kwanza
    • Huduma ya Pili
  • Councillors
  • Miradi
    • Mradi iliyokamilika
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Taarifa
    • Matukio
  • Divisheni

TAMASHA la kumbukizi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji kufanyika Songea kwa siku sita

Posted on: February 23rd, 2021


TAMASHA la kumbukizi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji linafanyika kwa siku sita katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea.

Mhifadhi wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Adson Ndyanabo amesema tamasha hilo linaanza Februari 22 na kilele chake kinatarajiwa kuwa Februari 27 mwaka huu na kwamba katika tamasha hilo wadau watashiriki maonesho ya vyakula vya asili ya Mkoa wa Ruvuma.

Shughuli nyingine zitakazofanyika kwenye tamasha hilo amezitaja kuwa ni kazi za sanaa za mikono,maonesho ya vita ya Majimaji,mavazi ya asili,burudani za ngoma za asili,muziki na kufanyika magwaride ya heshima.

Ndyanabo ameitaja kaulimbiu katika tamasha la mwaka huu kuwa ni Maisha ya wazee wetu fahari yetu na kwamba mgeni rasmi  kenye kilele cha tamasha hilo Februari 27 anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa.

Hata hivyo amesema tamasha hilo linatarajiwa kuzinduliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Damas Ndumbaro sanjari na kuzindua vilabu vya Historia na uzalendo vilivyoanzishwa katika shule ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais Dkt.John Magufuli kuhakikisha vijana mashuleni wanapata elimu ya uzalendo na historia ya nchi kwa ujumla.

Amesema tamasha hilo pia linafanya kongamano la wadau kwa lengo la kupeana elimu,mila na utamaduni wa  Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla.

Akizungumzia historia ya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji,Mhifadhi huyo amesema Makumbusho ya Taifa  ya Majimaji yaliyopo Mahenge mjini Songea,ni miongoni mwa makumbusho saba ya Shirika la Makumbusho ya Taifa na vituo 91 vya kale vilivyopo nchini.

“Makumbusho ya  Majimaji yalianzishwa na kufunguliwa Julai 6,1980, na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt.Lawrence Gama,lengo la kuanzisha makumbusho hayo ni kutunza kumbukumbu ya historia ya vita ya Majimaji iliyoanza mwaka 1905 hadi 1907’’,alisisitiza.

 Amesema  Makumbusho hiyo imejengwa katika eneo ambalo mashujaa 67 walizikwa baada ya kunyongwa kikatili na wajerumani.

Amelitaja eneo hilo la mashujaa maarufu kama hero square kuwa kuna makaburi mawili ya mashujaa moja ni la halaiki ambalo wamezikwa mashujaa 66 katika kaburi moja baada ya kunyongwa na serikali ya wakoloni wa kijerumani Februari 27,1906.

Kwa mujibu wa Mhifadhi huyo,kaburi la pili lililopo kwenye makumbusho hayo ni la Jemedari wa wangoni,Nduna (Sub chief) Songea Mbano aliyenyongwa  Machi 2,1906 na kwamba Mji wa Songea umepewa jina la jemedari huyo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma








TAMASHA la kumbukizi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji linafanyika kwa siku sita katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea.

Mhifadhi wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Adson Ndyanabo amesema tamasha hilo linaanza Februari 22 na kilele chake kinatarajiwa kuwa Februari 27 mwaka huu na kwamba katika tamasha hilo wadau watashiriki maonesho ya vyakula vya asili ya Mkoa wa Ruvuma.

Shughuli nyingine zitakazofanyika kwenye tamasha hilo amezitaja kuwa ni kazi za sanaa za mikono,maonesho ya vita ya Majimaji,mavazi ya asili,burudani za ngoma za asili,muziki na kufanyika magwaride ya heshima.

Ndyanabo ameitaja kaulimbiu katika tamasha la mwaka huu kuwa ni Maisha ya wazee wetu fahari yetu na kwamba mgeni rasmi  kenye kilele cha tamasha hilo Februari 27 anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa.

Hata hivyo amesema tamasha hilo linatarajiwa kuzinduliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Damas Ndumbaro sanjari na kuzindua vilabu vya Historia na uzalendo vilivyoanzishwa katika shule ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais Dkt.John Magufuli kuhakikisha vijana mashuleni wanapata elimu ya uzalendo na historia ya nchi kwa ujumla.

Amesema tamasha hilo pia linafanya kongamano la wadau kwa lengo la kupeana elimu,mila na utamaduni wa  Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla.

Akizungumzia historia ya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji,Mhifadhi huyo amesema Makumbusho ya Taifa  ya Majimaji yaliyopo Mahenge mjini Songea,ni miongoni mwa makumbusho saba ya Shirika la Makumbusho ya Taifa na vituo 91 vya kale vilivyopo nchini.

“Makumbusho ya  Majimaji yalianzishwa na kufunguliwa Julai 6,1980, na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt.Lawrence Gama,lengo la kuanzisha makumbusho hayo ni kutunza kumbukumbu ya historia ya vita ya Majimaji iliyoanza mwaka 1905 hadi 1907’’,alisisitiza.

 Amesema  Makumbusho hiyo imejengwa katika eneo ambalo mashujaa 67 walizikwa baada ya kunyongwa kikatili na wajerumani.

Amelitaja eneo hilo la mashujaa maarufu kama hero square kuwa kuna makaburi mawili ya mashujaa moja ni la halaiki ambalo wamezikwa mashujaa 66 katika kaburi moja baada ya kunyongwa na serikali ya wakoloni wa kijerumani Februari 27,1906.

Kwa mujibu wa Mhifadhi huyo,kaburi la pili lililopo kwenye makumbusho hayo ni la Jemedari wa wangoni,Nduna (Sub chief) Songea Mbano aliyenyongwa  Machi 2,1906 na kwamba Mji wa Songea umepewa jina la jemedari huyo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 22,2021






Matangazo

  • TANGAZO la vigezo vya kupata leseni ya biasharaJuly 31, 2021
  • TANGAZO la fursa za uwekezaji mkoani RuvumaMay 31, 2021
  • ILANI ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2020/2025May 31, 2021
  • Tazama zote



Habari Mpya

  • TAMASHA la kumbukizi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji kufanyika Songea kwa siku sita

    February 23, 2021


  •  
  • SERIKALI wilayani Songea yawaagiza wafanyabiashara waliogoma kurudisha huduma ndani ya saa 24

    February 22, 2021


  •  
  • BWAWA la umeme wa maji la Nyerere kujazwa maji Novemba 2021

    February 22, 2021


  •  
  • RAIS Magufuli afafanua vita ya corona

    February 22, 2021


  • Tazama zote


























TAMASHA la kumbukizi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji linafanyika kwa siku sita katika viwanja vya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji mjini Songea.

Mhifadhi wa Makumbusho ya Taifa ya Majimaji Adson Ndyanabo amesema tamasha hilo linaanza Februari 22 na kilele chake kinatarajiwa kuwa Februari 27 mwaka huu na kwamba katika tamasha hilo wadau watashiriki maonesho ya vyakula vya asili ya Mkoa wa Ruvuma.

Shughuli nyingine zitakazofanyika kwenye tamasha hilo amezitaja kuwa ni kazi za sanaa za mikono,maonesho ya vita ya Majimaji,mavazi ya asili,burudani za ngoma za asili,muziki na kufanyika magwaride ya heshima.

Ndyanabo ameitaja kaulimbiu katika tamasha la mwaka huu kuwa ni Maisha ya wazee wetu fahari yetu na kwamba mgeni rasmi  kenye kilele cha tamasha hilo Februari 27 anatarajiwa kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania Kassim Majaliwa.

Hata hivyo amesema tamasha hilo linatarajiwa kuzinduliwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt.Damas Ndumbaro sanjari na kuzindua vilabu vya Historia na uzalendo vilivyoanzishwa katika shule ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Rais Dkt.John Magufuli kuhakikisha vijana mashuleni wanapata elimu ya uzalendo na historia ya nchi kwa ujumla.

Amesema tamasha hilo pia linafanya kongamano la wadau kwa lengo la kupeana elimu,mila na utamaduni wa  Mkoa wa Ruvuma na Taifa kwa ujumla.

Akizungumzia historia ya Makumbusho ya Taifa ya Majimaji,Mhifadhi huyo amesema Makumbusho ya Taifa  ya Majimaji yaliyopo Mahenge mjini Songea,ni miongoni mwa makumbusho saba ya Shirika la Makumbusho ya Taifa na vituo 91 vya kale vilivyopo nchini.

“Makumbusho ya  Majimaji yalianzishwa na kufunguliwa Julai 6,1980, na aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Dkt.Lawrence Gama,lengo la kuanzisha makumbusho hayo ni kutunza kumbukumbu ya historia ya vita ya Majimaji iliyoanza mwaka 1905 hadi 1907’’,alisisitiza.

 Amesema  Makumbusho hiyo imejengwa katika eneo ambalo mashujaa 67 walizikwa baada ya kunyongwa kikatili na wajerumani.

Amelitaja eneo hilo la mashujaa maarufu kama hero square kuwa kuna makaburi mawili ya mashujaa moja ni la halaiki ambalo wamezikwa mashujaa 66 katika kaburi moja baada ya kunyongwa na serikali ya wakoloni wa kijerumani Februari 27,1906.

Kwa mujibu wa Mhifadhi huyo,kaburi la pili lililopo kwenye makumbusho hayo ni la Jemedari wa wangoni,Nduna (Sub chief) Songea Mbano aliyenyongwa  Machi 2,1906 na kwamba Mji wa Songea umepewa jina la jemedari huyo.

Imeandikwa na Albano Midelo

Afisa Habari Mkoa wa Ruvuma

Februari 22,2021






Matangazo

  • TANGAZO la vigezo vya kupata leseni ya biasharaJuly 31, 2021
  • TANGAZO la fursa za uwekezaji mkoani RuvumaMay 31, 2021
  • ILANI ya Chama Cha Mapinduzi CCM ya mwaka 2020/2025May 31, 2021
  • Tazama zote



Habari Mpya

  • TAMASHA la kumbukizi ya miaka 114 ya vita ya Majimaji kufanyika Songea kwa siku sita

    February 23, 2021


  •  
  • SERIKALI wilayani Songea yawaagiza wafanyabiashara waliogoma kurudisha huduma ndani ya saa 24

    February 22, 2021


  •  
  • BWAWA la umeme wa maji la Nyerere kujazwa maji Novemba 2021

    February 22, 2021


  •  
  • RAIS Magufuli afafanua vita ya corona

    February 22, 2021


  • Tazama zote






















Matangazo

  • VIGEZO vya kupata Lesen May 17, 2022
  • Angalia zote

Matangazo Mapya

  • Uboreshaji wa Daftari la kudumu jimbo la Madaba

    January 20, 2025
  • Jitokeze kujiandikisha

    January 20, 2025
  • Chwaya atoa rai kwa walimu wa awali kutekeleza agizo la Serikali

    January 18, 2025
  • MARATIBU wa mradi wa BOOST Madaba amshukuru Rais Samia

    January 18, 2025
  • Angalia zote

Video

WADAU WATOA MAONI JUU YA MAADILI KWA VIJANA
Video zaidi

Kurasa za karibu

  • Ruvuma-webportal
  • Mbinga District Council
  • Tunduru District Council
  • Nyasa District Council
  • Ega Website
  • Namtumbo District Council
  • Mbinga Town Cuncil
  • Songea District Council
  • Songea Municipal Council

Kurasa Mashuhuru

  • NECTA
  • Tanzania Revenue Authority
  • Tanzania Forest Agency
  • Watumishi portal
  • Livestock Training Agency (LITA) Madaba
  • Parliament

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

free HitCounter

Ramani ya Mahali

Wasiliana Nasi

    MADABA - RUVUMA

    Anwani ya Posta: 38 BARABARA YA KIFAGURO MAGINGO, P.O.BOX 10, 57186 MADABA, SONGEA

    Simu: 0252951052

    Simu ya Mkononi:

    Barua pepe: ded@madabadc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Falagha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani ya Mahali
    • Huduma

Hatimiliki@2017 Halmashauri ya Wilaya ya Madaba.Haki zote zimeifadhiwa